Mtandao wa
Wanafunzi Tanzania(TSN) wameiomba Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu
(HESLB) kushughulikia baadhi ya vipengele vinavyozungumzia sifa za mwanafunzi
anayepaswa kupata mikopo, kwa maelezo ni kandamizi na vinawanyima fursa
wanafunzi .
Moja ya
kipengele hicho ni kile cha mwanafunzi ambaye ana mzazi au mlezi
ayemiliki biashara au kampuni inayotambulika na mamlaka za usajili,
kutoruhusiwa kuomba mkopo
Akizungumza
leo Mkuu wa Idara ya Haki ya Wanafunzi wa mtandao huo, Gibson Eliaform amesema,
“Meneja ni cheo tu hakitambulishi uwezo wa mtu hata mwenye kibanda cha huduma
za fedha kwa mitandao ya simu na kampuni ndogo iliyosajiliwa anaweza kuwa
meneja wa biashara.”
“Anaweza kuwa
amesajili biashara yake Brela (Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ) au TRA
(Mamlaka ya Mapato Tanzania) na ana mtaji wa Sh500,000 je huyu ni tajiri?”
amehoji.
Amesema kipengele kingine ni kinachozuia
wanafunzi waliotajwa katika sheria ya utumishi wa umma kutoomba mikopo, ikiwamo
madiwani, maofisa watendaji wa kata na mtaa ambapo kimsingi kazi yao haina
mshahara.
Eliaform amesema kigezo hicho hakipo kisheria
na huenda kimewekwa makusudi ili kupunguza wanufaika wa mikopo kulingana na
bajeti
Amesema
kipengele kingine kinachotakiwa kufanyia marekebisho ni kuzuiwa wanafunzi
waliosoma shule binafsi, kubainisha kusoma shule binafsi siyo kigezo
kinachotambulisha uwezo wa mzazi kuhimili gharama za masomo Chuo Kikuu
“Hali
hubadilika kuna kufilisika, magonjwa na pia wanaolipa ada ndogo chini ya Sh1
milioni kuwanyima mikopo ni kukatisha ndoto zao,” amesema.
Mtandao wa wanafunzi wageuka mbogo masharti ya mikopo elimu ya juu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment