AG asema Kigwangalla hajavunja sheria kufuta vitalu vya uwindaji

 Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dk Adelardus Kilangi amesema Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla hajavunja sheria wala kanuni alipofuta vibali vya vitalu vya uwindani
 
Dk Kilangi ametoa kauli hiyo leo Mei 22, 2018 bungeni wakati akijibu hoja za baadhi ya wabunge ikiwemo kamati ya Bunge ya Ardhi, Utalii na Mazingira waliomtuhumu Dk Kigwangalla kuvunja sheria kwa kuvifuta vitalu 18

 “Waziri (Dk Kigwangalla) hakuvunja sheria alipochukua hatua hizi na imeelezwa vizuri katika barua ya Januari na mawasiliano mengine ya Oktoba na Desemba, alikuwa anachukua ili kuweka mfumo mzuri wa uendeshaji wa vitalu ili Taifa liweze kunufaika zaidi,” amesema Dk Kilangi
Mwanasheria huyo amesema Julai mwaka, 2017, Bunge lilitunga sheria ya usimamizi wa rasilimali za nchi, “Lakini ilikuwa ni kuhusisha Ibara ya 9 na 27 za Katiba ya Tanzania. Sehemu hii ya Katiba inahitaji sheria kuweza kuzitekeleza na mheshimiwa waziri hakuvunja sheria yoyote.”

Hata hivyo, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema, “Haya yanayojitokeza ni kipindi cha mpito. Siwezi kusema waziri amevunja sheria au hajavunja ninachoweza kusema ni kipindi cha mpito, ushauri wa AG utabaki kama ulivyo.”

Kuhusu mifugo kukamatwa inapoingia hifadhini, Profesa Kabudi amesema, “Hili ni suala nyeti, suala zito na Serikali imelisikia jambo hili na kulizingatia. Kesi nyingi ziko kwa Mkurugenzi wa Mashtaka na alipokea kesi zote.

AG asema Kigwangalla hajavunja sheria kufuta vitalu vya uwindaji AG asema Kigwangalla hajavunja sheria kufuta vitalu vya uwindaji Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: