MWAKYEMBE;TUSIPOTUMIA FURSA ZETU NCHINI WATU KUTOKA NJE WATAZIONA NA KUZICHANGAMKIA


Waziri wa habari sanaa  michezo na utamaduni Dokta Harson Mwakyembe amewataka watanzania kutumia fursa zilizopo kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa maarifa ili kuweza kujiingizia kipato  na kuongeza pato la taifa na hatiye kufikia uchumi wa kati.

Dokta mwakyembe ametoa rai hiyo wakati akifungua jukwaa la fursa za biashara Mkoani Arusha ambapo amesema kuwa pamoja na changamoto zilizopo ni vema watanzania wakafanya kazi kwa biidii kwa kugeuza changamoto hizo kuwa fursa kwani wasipotumia fursa hizo ipasavyo watu wengine kutoka nje wataziona kuzichangamkia.

Ameeleza jukwaa hilo ni mahususi kwa ajili ya kuhamasisha hari kwa kuchangamsha shughuli za kiuchumi Mkoani hapa ili kuufanya kuwa namba Moja katika kuvutia wawekezaji ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi na wageni kutumia fursa zilizopo ambapo iwapo jukwaa hilo litatumika vizuri litaweza kuvutia wawekezaji wengi zaidi ndani na nje ya nchi

Dokta Jim Yonazi Mhariri mtendaji wa kampuni ya magazeti ya serikali (TSN) ambapo ni waandaji jukwaa hilo amesema kuwa wameiangalia Tanzania kama nchi inayopiga kazi ya maendeleo hivyo wanahamasisha kwa kushiriki  kwa vitendo ili kuweza kuibua  fursa na kuzipeleka kwa wadaukupitia jukwaa hilo ili nchi iweze kuendelea na kufikia uchumi wa kati.

Kwa upande wake Moses Mabula mchumi Mkuu wa ofisi ya Mkoa wa Arusha amesema kuwa pato la Mkoa limepanda  kutoka trilioni 2.3 hadi trillion 4.2 na imefanikisha kuwa ya 7 kwa uchangiaji wa pato la taifa na kuwa ya 3 kwa ongezeko la pato la mkazi kutoka billion 1.2 hadi kufikia billion 2.3.

Naye Ester Ally Mtwalizya ameeleza kuwa jukwaa hilo litasaidia wajasiriamali kutangaza bidhaa zao ndani na nje ya Mkoa ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu hali itayofanya wasonge mbele.


MWAKYEMBE;TUSIPOTUMIA FURSA ZETU NCHINI WATU KUTOKA NJE WATAZIONA NA KUZICHANGAMKIA MWAKYEMBE;TUSIPOTUMIA FURSA ZETU NCHINI WATU KUTOKA NJE WATAZIONA NA KUZICHANGAMKIA Reviewed by KUSAGANEWS on May 24, 2018 Rating: 5

No comments: