Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imetoa
tahadhari ya kunyesha mvua kubwa kwa siku tano kuanzia leo, ambazo zinaweza
kuleta mafuriko katika maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi,
Mtwara na Visiwa vya Unguja na Pemba
Katika taarifa ya TMA iliyotolewa leo Mei
13, mvua hizo zilizoanza kunyesha leo, zitaendelea mpaka Mei 17 mwaka huu
TMA imesema athari zinazinaweza kutokea
ikiwemo mafuriko ambayo yanaweza kusababisha kuvurugika kwa usafiri, barabara
kubwa kutopitika na maisha ya watu kuwa hatarini kutokana na maji kujaa
au kupita kwa kasi
Pia imetoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo
kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari
zitakazotolewa
Mvua bado ipo ipo sana
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 13, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment