Makhtar Diop, raia wa Senegal ameteuliwa
kuwa makamu wa rais wa Benki ya Dunia (WB) atakayekuwa anasimamia miundombinu
Diop alitangazwa kushika nafasi hiyo
mwishoni mwa wiki iliyopita na hivyo kumfanya kuwa miongoni mwa maofisa wa
ngazi za juu wa taasisi hiyo muhimu duniani
Taarifa iliyotolewa na benki hiyo inasema
Diop anayaanza majukumu hayo mapya baada ya kuwa Makamu wa Rais anayesimamia
Afrika katika miaka sita iliyopita akifanikisha kutolewa kwa mikopo yenye
thamani ya Dola 70 bilioni za Marekani
Ndani ya miaka hiyo sita, Diop alisimamia
miundombinu ya usafiri na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), nishati
na madini, fedha na ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi (PPP
‘Katika majukumu yake mapya, Diop atasimamia
ufadhili wa miundombinu ya fedha katika ufanikishaji wa maendeleo endelevu
hivyo kupunguza tofauti iliyopo kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea,”
inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.
Uteuzi wa Diop anayetajwa kuwa miongoni mwa
Waafrika 100 wenye ushawishi zaidi duniani utaanza Julai Mosi
Alipokuwa akiisimamia Afrika, inaelezwa
alisimamia upatikanaji wa fedha za kufanikisha miradi ya aina tofauti
akihamasisha zaidi ubunifu na uvumbuzi wa kisayansi
Alihakikisha Afrika inapata umeme wa uhakika
na nafuu huku ikiunganishwa kwa barabara zinazopitika wakati wote
Ndani ya benki hiyo, Diop ameshahudumu kama mkurugenzi wa fedha, sekta binafsi na miundombinu Amerika Kusini na Visiwa vya Caribbean
Kati ya mwaka 2009 na 2012 alikuwa
mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia, Brazil ambako alisimamia utekelezaji wa
miradi mikubwa ya maendeleo
Alishawahi kuwa Mkurugenzi Mkazi katika nchi za Kenya, Eritrea na Somalia.
Msenegal ateuliwa makamu rais Benki ya Dunia
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 13, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment