Mahakama Kuu
Kanda ya Moshi, leo itatoa uamuzi wa iwapo washtakiwa saba katika kesi ya
mauaji ya kukusudia ya mfanyabiashara Erasto Msuya kama wana kesi ya kujibu au
la
Uamuzi huo
utatolewa na Jaji Salma Maghimbi anayesikiliza kesi hiyo, baada ya upande wa
mashtaka ukiongozwa na wakili mwandamizi wa Serikali, Abdallah Chavulla kufunga
ushahidi. Iwapo Jaji Maghimbi ataona yupo mshtakiwa ambaye hana kesi ya kujibu
atamwachia huru, lakini kwa watakaoonekana wana kesi ya kujibu, itawalazimu
kujitetea
Msuya
aliyekuwa akimiliki vitega uchumi kadhaa ndani na nje ya Arusha, aliuawa kwa
kupigwa risasi Agosti 7, 2013 eneo la Mijohoroni wilayani Hai
Kesi hiyo
inayovuta hisia za wengi inawakabili washtakiwa saba ambao ni Sharifu Mohamed,
Shaibu Jumanne, Mussa Mangu, Jalila Zuberi, Karim Kihundwa, Sadick Jabir na
Ally Mussa. Awali, upande wa mashtaka ulieleza ungekuwa na mashahidi 50 lakini
hadi ulipofunga ushahidi Ijumaa iliyopita, walileta mashahidi 27 na vielelezo
27 viliwasilishwa mahakamani.
Jaji kutoa mwelekeo kesi ya bilionea Msuya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 13, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment