Museveni awashtumu madaktari waliogoma

Sembabule, Uganda. Rais Yoweri Museveni amezungumzia suala la mgomo wa madaktari na kwa hasira amewaita wote walioweka vifaa chini mwishoni mwa mwaka jana kuwa ni “maadui wa Uganda wanaopaswa kuchukuliwa hivyo.”

Madaktari kote nchini waligoma kwa wiki tatu Novemba mwaka jana wakishinikiza Serikali kutekeleza lundo la matakwa yao ambayo ni kuboresha mishahara yao na marupurupu ya nyumba, magari, wafanyakazi wa nyumbani na kufanyiwa mageuzi kitengo cha kusimamia afya cha Ikulu

Masuala mengine muhimu ambayo madaktari walihitaji ni upatikanaji wa uhakika wa dawa, huduma nzuri na mafunzo bora kwa wanafunzi wa udaktari

Mgomo ule ulisababisha huduma za afya kudorora nchini na wagonjwa wengi walikufa kutokana na ukosefu wa huduma au kucheleweshewa matibabu

Mkwamo huo wa huduma za afya ulisababisha Serikali kuingia katika mpango uliopingwa wa kuagiza madaktari 200 kutoka Cuba kuchukua nafasi za waliogoma

Lakini, akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani akiwa katika Wilaya ya Sembabule, Museveni kwa ari kubwa alitetea uamuzi tata wa Serikali wa kuagiza madaktari kutoka nje akiwashtumu madaktari wazawa kwa usaliti na “kuonyesha tabia mbaya na kinyume cha taaluma”.



Museveni awashtumu madaktari waliogoma Museveni awashtumu madaktari waliogoma Reviewed by KUSAGANEWS on May 02, 2018 Rating: 5

No comments: