Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM Sumbawanga auawa kwa kupigwa risasi


Mtendaji wa Kata ya Mwandui iliyopo mwambao wa bonde la ziwa Rukwa, wilayani Sumbawanga mkoani hapa, Benedict Chapewa ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando amesema tukio hilo limetokea   usiku wa kuamkia leo, Mei 3
Kamanda Kyando amesema kuwa Chapewa ambaye amewahi kuwa Katibu Mwenezi, CCM Wilaya ya Sumbawanga, alivamiwa na kundi la watu wasiojulikana wakati akiwa anakunywa pombe katika moja ya baa anayomiliki kijijini hapo

“Watu hao walimmiminia risasi kwa kutumia bunduki aina ya gobore kisha kumkata kata na mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake,” amesema

Amesema baada ya wauaji kutekeleza adhima yao waliondoka kuelekea kusikojulikana na hawakuchukua kitu chochote kutoka kwa marehemu au katika baa hiyo

Kamanda Kyando amesema uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo unaendelea kufanyika na watuhumiwa wanasakwa popote walipo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake

Ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi kwani kufanya hivyo ni ukiukaji wa haki za binadamu na vyombo vya dola vitahakikisha vinawachukulia hatua za kisheria wale wote wanajichukulia sheria mkononi.
Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM Sumbawanga auawa kwa kupigwa risasi Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM Sumbawanga auawa kwa kupigwa risasi Reviewed by KUSAGANEWS on May 02, 2018 Rating: 5

No comments: