Miujiza ya Mwijage yamuacha hewani Bashe

Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), amesema mfumo wa kodi nchini umesababisha gharama za uzalishaji bidhaa kuongezeka na kudumaza mazingira rafiki ya uwekezaji na kwamba hata miujiza aliyokuwa akisubiri kuiona mpaka sasa haijatokea.
Bashe ametoa kauli hiyo leo bungeni , wakati akichangia mjadala wa bajeti na kuongeza kuwa licha ya mwaka 2016 kumwambia Waziri wa Viwanda, Uwekezaji na Biashara, Charles Mwijage kuwa anasubiri aone miujiza katika wizara hiyo, hadi sasa inashangaza kuona hakuna kilichotokea.

Mbunge huyo  ameitaka Wizara hiyo, kukutana na Wizara ya Fedha na Mipango ili kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji yatakayomsaidia Rais John Magufuli kutimiza ndoto ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.

Muujiza wa kwanza ulikuwa ni kuona namna gani Wizara ya Viwanda inaweza kuunganisha mambo matatu ambayo amekabidhiwa. Rais aliamua kwa makusudi kuunganisha biashara, viwanda na uwekezaji ili kufikia lengo la mapinduzi ya viwanda, lakini hadi leo tunazungumzia General Tyre, Liganga na Mchuchuma. Kuna matatizo ya msingi ya biashara lakini huoni kwenye mpango wetu namna ya kuyashughlikia,” amesema.

Amesema licha ya Mwijage kutaja vipaumbele vya wizara hiyo kwa mwaka 2018/19, hakuna mpango unaoonesha kuondoa matatizo yaliyopo kwenye mifumo ya kodi, miongozo na sheria katika kufanya biashara nchini.

Miujiza ya Mwijage yamuacha hewani Bashe Miujiza ya Mwijage yamuacha hewani Bashe Reviewed by KUSAGANEWS on May 11, 2018 Rating: 5

No comments: