IGP awataka polisi kujenga umoja na wananchi

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro ameagiza Watumishi wa jeshi hilo kufanya majukumu yao kwa kuzingatia utii wa sheria ili kujenga umoja baina yao na wananchi. 

Ameyasema hayo mara baada ya kushiriki gwaride la kuwaaga Makamishana wa Polisi Alice Mapunda Kamisheni ya uchunguzi wa kisayansi wa makosa ya jinai na Kamishna Mstaafu Fedha na lojistiki Clodwig Mtweve kwenye viwanja vya chuo cha Polisi Kurasini.

IGP Sirro amesema ni wajibu wa kila mtu kuhakikisha anakua mtiifu katika utendaji kazi wao wa kila siku.

Kwa upande wao Makamishna wastaafu kwa pamoja wamewataka watenda kazi wa jeshi hilo kutekeleza kazi zao kwa uweledi na kujenga ukaribu na wananchi ili kubaini vitu vingi ambavyo ni msaada kwa majukumu yao..

IGP awataka polisi kujenga umoja na wananchi IGP awataka polisi kujenga umoja na wananchi Reviewed by KUSAGANEWS on May 11, 2018 Rating: 5

No comments: