Mhagama ataka sera, sheria zitizamwe upya


Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama amesema katika kujenga uchumi wa viwanda bado Serikali inatakiwa kutazama upya sheria na sera

Akizungumza leo Mei 25, 2018 jijini Dodoma katika mkutano wa kuhamasisha ushiriki wa wazawa katika uchumi wa viwanda, Waziri Mhagama amesema anasimamia kikamilifu suala hilo

Amesema kila sheria inayopita bungeni amekuwa akiuliza maudhui ya ushiriki wa wazawa kwenye sheria yenyewe ama kwenye kanuni

“Kwa sababu msingi ukiwekwa katika sheria ni lazima kanuni itafsiri jambo hilo vizuri. Sisi kama Serikali utayari wetu ni mkubwa sana,”amesema

Amesema dhana ya ushiriki wa wazawa itakapotekelezwa katika miradi mikubwa inayofanywa na watu kutoka nje ya nchi lazima Watanzania watapata ujuzi

“Ninaiona Tanzania mpya kupitia mkakati Local content mnaokwenda kuitayarisha. Naisubiri kwa hamu. Sera za namna hii zikitekelezwa zitachangia kukuza viwanda na makampuni ya ndani ya nchi yetu,”amesema Mhagama

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji (NEEC), Being’I Issa ambao ndio waandaaji wa mkutano huo wakishirikiana na Taasisi ya Uongozi amesema bado bidhaa zinazouzwa kwa wawekezaji nchini ni chache

Pia amesema ushiriki wa wazawa wengi katika miradi mikubwa bado ni kwenye ujuzi wa chini na hivyo kutaka kujengewa uwezo

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uongozi Nchini, Joseph Semboja ametaka uwezeshaji wa wazawa ili waweze kunufaika na fursa zinazotokana na miradi mikubwa nchini.

Mhagama ataka sera, sheria zitizamwe upya Mhagama ataka sera, sheria zitizamwe upya Reviewed by KUSAGANEWS on May 25, 2018 Rating: 5

No comments: