Idara ya wagonjwa Mahututi Bugando yakabiliwa na upungufu wa Madaktari


Idara ya wagonjwa Mahututi katika hospitali ya rufaa Bugando, inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa, vifaa tiba ikiwa na sehemu finyu ya kupokelea wagonjwa zaidi ya 100 ambao wamekuwa wakifikishwa katika idara hiyo kila siku

Mkurugenzi Mkuu wa hospitali hiyo Dkt. ABEL MAKUBI Ameeleza changamoto hizo wakati akipokea hundi ya shilingi milioni 240 iliyotolewa kama msaada na benki ya CRDB nchini kwa ajili ya kuunga mkono upanuzi wa ujenzi wa idara ya wagonjwa mahtuti, katika tukio lililohudhuriwa na maaskofu wakuu watatu wa majimbo makuu ya Songea, Dodoma na Mwanza

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi mkuu wa benki ya CRDB ESTER KILEO amesema benki hiyo imekuwa na ushirikiano mkubwa na hospitali hiyo katika kuboresha mazingira ya utoaji tiba, na hii ikiwa ni mara ya pili katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ambapo mwaka 2013, benki hiyo ilifanya ukarabati wa wodi ya wazazi, kutoa vifaa mbalimbali vya tiba pamoja na kupanda miti zaidi ya 100, msaada uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 55

Mwenyekiti wa bodi ya hospitali ya rufaa ya kanda ya ziwa Bugando, ambaye pia ni Askofu mkuu wa jimbo kuu la Mwanza Mhashamu YUDA THADEI RWAICHI ameipongeza benki hiyo kwa utayari na ushiriki wao katika masuala ya huduma za kijamii na kwa moyo wao wa matendo ya huruma na wema katika kumhudumia mwanadamu kimwili.
Idara ya wagonjwa Mahututi Bugando yakabiliwa na upungufu wa Madaktari Idara ya wagonjwa Mahututi Bugando yakabiliwa na upungufu wa Madaktari Reviewed by KUSAGANEWS on May 25, 2018 Rating: 5

No comments: