Mbatia ataka wimbo wa Taifa utumike kudumisha umoja nchini


Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amewashauri viongozi mbalimbali nchini, kuutumia wimbo wa Taifa kuongoza ili kudumisha umoja

Mwenyekiti huyo wa  NCCR-Mageuzi, ametoa ushauri huo leo bungeni Mei 22, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2018/19.

Katika mchango wake, Mbatia amegusia mazingira yasiyo rafiki ya utalii na mikakati isiyoonyesha mwanga ya kuutangaza ndani na nje ya nchi, huku akisema asilimia 98 ya mapato yanayotokana na utalii yanatoka mikoa ya kaskazini mwa Tanzania

“Kuna kiongozi nilimsikia akisema watu wa kaskazini wasubiri kwanza.  Zaburi 141:3 inasema ‘Ee Mwenyezi-Mungu ukilinde kinywa changu, uweke ulinzi mlangoni mwa mdomo wangu’,” amesema Mbatia

Amesema kama asilimia 98 ya mapato ya utalii yanatoka mikoa ya kaskazini, inapaswa kujengewa uwezo ili iendelee kuwa juu

“Mama Tanzania anatuasa kuwa wamoja. Taifa hili ni moja, watu wengine wanaotoka Kaskazini tusianze kugawana kwa ukabila na ukanda. Tanzania ni yetu sote na wimbo wa Taifa unazungumzia hekima, umoja na amani ili tuweze kukuza utalii wetu, viongozi wazingatie huu wimbo,” amesema.

Mbatia ataka wimbo wa Taifa utumike kudumisha umoja nchini Mbatia ataka wimbo wa Taifa utumike kudumisha umoja nchini Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: