Madaktari wamsaidia mzee wa miaka 104 kujiua


Shirika linalotetea haki za watu wanaotaka kufa limetangaza kuwa mwanasayansi David Goodall, 104, aliyesafiri kutoka Australia hadi Uswizi ili kujitoa uhai amefariki katika kliniki moja nchini Uswizi.
 Mwanaikolojia huyo ambaye pia alikuwa mtaalamu wa mimea hakuwa anaugua lakini alisema aliamua kujitoa uhai kutokana na kudhoofika kwa 'ubora wa maisha yake'.
Goodall alikuwa amezua mjadala kutokana na safari yake ya kutoka Australia kwenda kujitoa uhai.
Muda mfupi kabla ya kifo chake, alisema alikuwa na "furaha kuhitimisha" maisha yake.
"Maisha yangu yamekuwa dhaifu sana kwa mwaka mmoja hivi uliopita na hivyo basi nina furaha kuyahitimisha," alisema akiwa amezingirwa na jamaa wake kadha.
"Nafikiria, kuangaziwa kwa kisa changu kutachangia kutetea haki za wazee kuruhusiwa kujitoa uhai, jambo ambalo nimekuwa nikitaka."
Alifariki leo saa sita na nusu mchana katika kliniki ya Life Cycle mjini Basel baada ya kudungwa sindano ya Nembutal, kwa mujibu wa Philip Nitschke mwanzilishi wa shirika la Exit International lililomsaidia kujitoa uhai.
"Najuta kufika umri huu," Dkt Goodall alisema mwezi uliopita katika sherehe ya kuzaliwa kwake, katika mahojiano na shirika la utangazaji la Australia.
Aliyedaiwa kufariki azinduka akiwa chumba cha kuhifadhia maiti
"Sina raha. Nataka kufa. Sio jambo la kuhuzunisha, kinachohuzunisha ni kwamba mtu anazuiwa kufa."
Ni jimbo moja pekee Australia lililohalalisha kujitoa uhai mwaka jana kufuatia mjadala mkali uliozusha mgawanyiko, lakini ili mtu kuruhusiwa, ni sharti awe anaugua mahututi.

Madaktari wamsaidia mzee wa miaka 104 kujiua Madaktari wamsaidia mzee wa miaka 104 kujiua Reviewed by KUSAGANEWS on May 10, 2018 Rating: 5

No comments: