Mbunge wa
Ubungo (Chadema), Saed Kubenea ameuweka rehani mshahara wake wa ubunge wa Mei,
2018 akitaka apatiwe mbunge wa CCM atakayesimama na kupinga bajeti ya Wizara ya
Mifugo na Uvuvi mwaka 2018/19, inayotarajiwa kupitishwa leo Ijumaa jioni Mei
18, 2018
Kubenea ametoa
kauli hiyo leo bungeni mjini Dodoma katika mjadala wa bajeti hiyo , kubainisha
kuwa wabunge wa CCM wamekuwa wakipitisha kwa nguvu bajeti baada ya kuitwa
kwenye vikao vya ndani vya chama hicho
Baada ya
Kubenea kueleza hayo, baadaye Spika wa Bunge, Job ndugai aliwatangazia
wabunge wa chama hicho tawala kuwa watakuwa na kikao cha ndani
kitakachofanyika katika ukumbi wa White House, kabla ya kurejea tena bungeni
saa 10 jioni
Mara nyingi
hoja za wabunge zinapokuwa moto bungeni kuhusu wizara fulani, CCM huitisha
vikao hivyo vya ndani
“Mheshimiwa
Spika kama atasimama mbunge yeyote wa CCM na kutaka kukwamisha bajeti hii,
natangaza mshahara wangu wa mwezi huu apewe akaongezee bajeti yake, huwa
mnatupiga maneno tu bila vitendo,” amesema Kubenea
Amesema ni
aibu kwa Serikali kuendelea kuagiza nyama, kuku na samaki kutoka nje ya nchi
wakati vitu hivyo vimejaa nchini
Kubenea: Mbunge wa CCM atakayepinga bajeti Wizara ya Mifugo na Uvuvi, apewe mshahara wangu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 18, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment