Kagera kuna upungufu wa vyumba vya madarasa 8,341


Mkoa wa Kagera umetajwa kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 8,341 vya shule za msingi sawa na asilimia 58, Bunge limeelezwa leo Jumanne Mei 22, 2018. Mkoa huo una mahitaji ya vyumba vya madarasa 14,275 lakini vilivyopo ni 5,934.

 Akizungumza bungeni leo Naibu Waziri wa Tamisemi, Josephat Kandege amesema kuwa katika mkoa huo pia kuna mahitaji ya ofisi za walimu 1,780, kwamba zilizopo ni 925 na hivyo kuwa na upungufu wa ofisi 855 ambayo ni asilimia 48

Kandege ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum (CUF), Alfredina Kahigi aliyetaka kujua Serikali inawasaidiaje wanafunzi wa mkoa huo kupata mahali pazuri pa kusomea pamoja na walimu kupata ofisi nzuri ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa.

 Katika maelezo yake naibu waziri huyo amesema kwa shule za sekondari  kuna mahitaji ya vyumba vya madarasa 2,379, vilivyopo ni i 1,582.

“Kwa sekondari kuna upungufu wa vyumba  797 vya madarasawa  sawa na asilimia 34. Majengo ya utawala yanayohitajika ni 212, yaliyopo sasa ni 67 na hivyo kusababisha upungufu wa majengo 145 ambao ni asilimia 68,” amesema.

Naibu Waziri amesema upungufu pia umejitokeza katika miundombinu mingine zikiwemo nyumba za walimu, vyoo na maabara na tayari Serikali imefanya mikakati mbalimbali kuhakikisha kuwa wanafunzi na walimu katika mkoa huo na Taifa wanapata mahali pazuri pa kusomea

Kagera kuna upungufu wa vyumba vya madarasa 8,341 Kagera kuna upungufu wa vyumba vya madarasa 8,341 Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: