Mradi wa maji kutoka Ziwa Tanganyika kukamilika Juni mwaka huu


Serikali imeanza kutekeleza miradi ya maji kutoa maziwa makuu nchini kupeleka kwa wananchi wanaoishi karibu na maziwa hayo.

Katika Mkoa wa Kigoma, Serikali inatekeleza mradi unaogharimu S 42 bilioni kutoka Ziwa Tanganyika kwenda Manispaa ya Kigoma Ujiji huku utekelezaji wa mradi huo ukitarajiwa kukamilika Juni 2018

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Mei 22, 2018 na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso  wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalumu (CCM),  Silafu Jumbe Maufi aliyehoji Serikali kama haioni umuhimu wa kuanzisha mradi wa maji kutoka kwenye vyanzo hivyo na kusambaza kwa wananchi

Katika ufafanuzi wake naibu waziri huyo amesema Serikali  itaendelea na jitihada za kutumia vyanzo vya maji vya Ziwa Rukwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma.

 “Hivyo Wizara imeziagiza mamlaka za majisafi na usanifu wa miradi ya maji na uandaaji wa makablasha ya zabuni kwa ajili ya miradi ya maji itakayotumia vyanzo hivyo,” amesema Aweso
Kwa mujibu wa naibu waziri huyo, amesema utekelezaji wa miradi hiyo unafanyika kupitia programu ya maendeleo ya sekta ya maji awamu ya pili ya (WSDP II).
Mradi wa maji kutoka Ziwa Tanganyika kukamilika Juni mwaka huu Mradi wa maji kutoka Ziwa Tanganyika kukamilika Juni mwaka huu Reviewed by KUSAGANEWS on May 22, 2018 Rating: 5

No comments: