Siku 12 tangu
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alipoachiwa huru, jana aliingia bungeni na kusimamisha
shughuli za Bunge kwa dakika kadhaa
Sugu, ambaye
ni mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), alihudhuria kikao cha 33 cha Bunge la
Bajeti lililoanza Aprili 3 likitarajiwa kuhitimishwa Juni 29 akiwa amevaa suti
ya bluu bahari ikiwa na nembo ya namba yake ya mfungwa 219/2018.
Akiwa ameongozana na mbunge wa viti maalumu
(Chadema), Kunti Yusuph, Sugu alikanyaga lango la kuingia bungeni saa 3:16
asubuhi kabla ya kuingia ukumbini saa 3:20
Wakati
akiingia, mbunge huyo alipita katikati ya ukumbi na wabunge wa upinzani
walianza kumshangilia kwa kugonga meza. Awali alikosa vikao vya Bunge tangu
Novemba, mwaka jana
Wa kwanza
kusalimiana na mbunge huyo alikuwa mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye kisha
akapokewa na mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini kwa upande wa upinzani.
Sugu atinga bungeni na nembo ya namba yake ya mfungwa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment