Waziri
wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema licha ya utajiri wa rasilimali
uliopo nchini wananchi wameendelea kuwa maskini
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa taasisi ya utafiti wa uchumi na jamii
Dar es salaam, Dk Mpango aliyemwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaja
sababu kubwa kuwa ni kutokuwepo kwa uwiano kati ya ukuaji wa uchumi na sekta ya
Kilimo
Amesema Tanzania
ni tajiri wa rasilimali ikiwemo maziwa kama Victoria, Tanganyika, Rukwa, Nyasa
na mito mingi inayotoa fursa za uvuvi na uzalisha wa umeme pamoja utajiri wa
madini kama dhahabu, almasi, Tanzanite, ruby, bati, chuma, mkaa, uranium, gesi
ya asili, helium na mengineyo.
Ameongeza
kuwa Tanzania ni kituo kikubwa cha utalii ikiwa na urefu wa kilometa 1,200 za
fukwe za bahari, hifadhi za wanyama, huku ikiwa nchi ya amani na utulivu
isiyokuwa na machafuko ya kikabila
Hata
hivyo,Dokta Mpango amesema uporaji wa maliasili umesababisha maisha ya
Watanzania walio wengi kuwa masikini, huku wachache wakifaidi rasilimali hizo
Dk. Mpango akiri ongezeko la umaskini licha ya utajiri wa rasilimali
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 02, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment