Serikali imesema
itawachukulia hatua kali za kisheria wafanyabiashara wanaojihusisha na
usafirishaji wa watanzania kwenda nje ya nchi kufanya kazi endapo itabaini kuwa
wanawapeleka huko kuwauza miili yao nasio kuwaunganisha katika kazi rasmi kama
walivyokubaliana.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mei 21,
2018 na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Susan Kolimba Bungeni Jijini Dodoma
kwenye kikao cha 33 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, wakati akijibu la nyongeza la Mbunge Hawa Mchafu aliyetaka kufahamu
serikali imechukua hatua gani za kisheria dhidi ya wafanyabiashara
wanaosafirisha watanzania hususani vijana wa kike kwenda nje ya nchi kwa ajili
ya kufanya biashara isio rasmi ikiwemo kuuza miili yao.
"Kama taarifa hiyo itajulikana
kuwa ni kweli, hatua za kisheria za nchi yetu zitachukuliwa kwa watu
wanaojihusisha na vitendo hivyo lakini mpaka sasa mimi sina 'data' za aina
hiyo", amesema Dkt. Kolimba.
Mbali na jibu hilo Dkt. Kolimba
amesema yeye pamoja na Wizara yake watafuatilia madai ya watanzania
wanaosafirishwa kwenda na nje ya nchi na kuchukuliwa figo zao kuuzwa ili wapata
kuwachukulia hatu za kisheria kwa mawakala na watu wanaofanyabiashara ya
kusafirisha watanzania kwenda nje ya nchi kwa kigezo cha kufanya kazi.
Biashara ya kuwauza watanzania nje yatua Bungeni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 21, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 21, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment