Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
amefunguka na kusema kuwa familia 170 ambazo zilikwenda jana ofisini kwake
waliweza kuelewana namna ya kulea watoto wao na kusema zoezi linakwenda vizuri
kama ambavyo lilikusudiwa na kudai kuanzia Jumatatu sasa wataanza kuitwa wakina
baba.
Makonda amesema hayo April 12, 2018
wakati akiongea na waandishi wa habari na kutolea ufafanuzi juu ya masuala
mbalimbali ikiwepo watu ambao wamesema ni watoto wa viongozi fulani na
hawajafika ofisini kwake amewasihi kufika ofisi kwa kuwa wao wanafanya kazi na
watu ambao wamekwenda ofisini na si wale ambao wanajirekodi kwenye mitandao ya
jamii.
"Hatimaye tunaona familia
zinarudi katika msingi wake zoezi hili tunaendelea nalo leo na kesho tutaona
idadi tutakayoifikia kwani lengo tukishamalizana na kina mama Jumatatu
tutawaita wakina baba ambao wengine wameshaanza kuja na wengine tutawaita kwani
lengo la serikali ni kuhakikisha ustawi unaanzia kwenye familia" alisema Makonda
Aidha Makonda amesema kuwa watoto
ambao wametelekezwa na baba zao labda wapo nje ya Tanzania au wamefariki basi
watajitahidi kuhakikisha wanampunguzia machungu mama wa mtoto kwa
kuwaandikishia bima ya afya na kudai kuna mtu amejitolea zaidi milioni 250 kwa
ajili ya kuwakatia bima ya afya watoto hao.
Wiki ijayo zamu ya wababa - Paul Makonda
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment