Msanii wa muziki wa kizazi kipya
Nandy ambaye hi leo amekutwa na balaa la kuvuja kwa video yake ya utupu,
ameomba radhi kwa watu mbali mbali ikiwemo kanisa lake juu ya video hiyo,
inayomuonyesha akiwa faragha na msanii mwenzake Bill Nas.
Akizungumza hilo Nandy amesema video
hiyo ni ya mwaka 2016, na haelewi kwa nini mtu aliyeivujisha kaamua kufanya
hivyo, lakini ni kitendo kilichomuumiza sana hivyo anaomba msamaha kwa
jamii, mashabiki, kanisa na kila mtu ambaye imemgusa kwa namna moja au
nyingine wamsamehe, kwani tayari anajutia jambo hilo.
“Nimesikitika sana, hiyo video ni ya
ukweli ni ya mwaka 2016, nilikuwa na mahusiano na Bill Nas na
tulikubaliana iwe siri, sasa sielewi kwa sababu gani kaamua kuvujisha,
nimesikitishwa sana, ni video ambayo ilishutiwa kwa snapchat, sasa sielewi
wakati ameipata hiyo video alikuwa nayo au alichukua mwenyewe, sijui niseme
nini, naomba radhi sana kwa familia yangu, kanisani kwangu, serikali yangu,
mashabiki, naomba radhi sana, adhabu ya maumivu ambayo nayapata imetokana na
kumuamini mtu, ilikuwa ni private”, amesema Nandy.
Wawili hawa mara kwa mara walikuwa
na skendo ya kuwa na mahusiano lakini wamekuwa wakikanusha, na watu kuanza
kuibua hisia upya baada ya Nandy kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa Bill Nas kwa
kupost picha inayomuonyesha akiwa kifuani kwake.
Nandy aomba radhi mpaka kwa kanisa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment