Wazee, walemavu wapewa vitambulisho bima ya afya, kuingia mgodi wa Tanzanite


Wazee 305 na walemavu 24 wa mji mdogo wa Mirerani wilayani 
Simanjiro, wamepatiwa vitambulisho vitakavyowawezesha kupatiwa 
matibabu bure na kuingia ndani ya migodi ya madini ya Tanzanite
 
Watu hao walikabidhiwa vitambulisho hivyo jana mtaa wa Kazamoyo 
mji mdogo wa Mirerani na mkuu wa wilaya hiyo, Zephania Chaula.
 
Mwenyekiti wa sauti ya walemavu Mirerani, Robert Songa alisema 
kundi hilo maalumu linapaswa kuangaliwa kwa jicho la huruma kwenye 
sekta mbalimbali 
 
Songa alisema kupitia vitambulisho hivyo, walemavu hao wataingia 
ndani ya ukuta na kufanya shughuli zao, ikiwamo kuchekecha 
mchanga wakati wa utafutaji wa madini ya Tanzanite
 
“Mkuu wa wilaya na ofisa madini mkazi Mirerani, Frederick Girenga 
asanteni kwa kufanikisha sisi kupata vitambulisho hivi,” alisema 
Songa
 
Naye Chaula alisema Serikali inawajali wazee na walemavu ndiyo 
sababu wakawapa kipaumbele kwenye utoaji wa vitambulisho vya 
kupata matibabu bure na kuingia ndani ya ukuta
 
Chaula alisema hiyo ni awamu ya kwanza, hivi sasa wanajipanga 
kutoe kwa wazee na walemavu wengine ambao hawajavipata.
Wazee, walemavu wapewa vitambulisho bima ya afya, kuingia mgodi wa Tanzanite Wazee, walemavu wapewa vitambulisho bima ya afya, kuingia mgodi wa Tanzanite Reviewed by KUSAGANEWS on April 14, 2018 Rating: 5

No comments: