Serikali ya Syria,
imeimarisha mashambulizi makali usiku wa kuamkia Jumamosi, katika ngome ya
mwisho ya waasi karibu na mji mkuu Damascus nchini Syria, na kusababisha idadi
ya raia waliouawa kuongezeka na kufikia 40.
Kwa mujibu wa shirika la kutetea haki za binadamu Syria, mashambulizi hayo pia yameuvunja utulivu ambao umedumu mjini Douma kwa muda wa siku 10 zilizopita.
Mkuu wa shirika
linaloangalia haki za binadamu la Syria- Rami Abdel Rahman, ameeleza kuwa
mashambulizi hayo ni ya jazba na amezungumzia mamia ya operesheni zilizofanywa
Douma.
Abdel Rahman ameongeza
kuwa mashambulizi ya makombora kutoka angani yamefanywa sambamba na
mashambulizi ya ardhini ambayo yamefanywa na vikosi vya Syria, kusini magharibi
na mashariki mwa Douma.
WATU 40 WAUWAWA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment