WATU 40 WAUWAWA


Serikali ya Syria, imeimarisha mashambulizi makali usiku wa kuamkia Jumamosi, katika ngome ya mwisho ya waasi karibu na mji mkuu Damascus nchini Syria, na kusababisha idadi ya raia waliouawa kuongezeka na kufikia 40.

Kwa mujibu wa shirika la kutetea haki za binadamu Syria, mashambulizi hayo pia yameuvunja utulivu ambao umedumu mjini Douma kwa muda wa siku 10 zilizopita.

Mkuu wa shirika linaloangalia haki za binadamu la Syria- Rami Abdel Rahman, ameeleza kuwa mashambulizi hayo ni ya jazba na amezungumzia mamia ya operesheni zilizofanywa Douma.

Abdel Rahman ameongeza kuwa mashambulizi ya makombora kutoka angani yamefanywa sambamba na mashambulizi ya ardhini ambayo yamefanywa na vikosi vya Syria, kusini magharibi na mashariki mwa Douma.

WATU 40 WAUWAWA WATU 40 WAUWAWA Reviewed by KUSAGANEWS on April 07, 2018 Rating: 5

No comments: