Mkuu wa wilaya ya Arusha Mjini Mh Fabian Daqaro amezitaka kaya maskini katika
jiji la Arusha zinazonufaika na Fedha za TASAF awamu ya tatu kuzitumia vizuri
ili ziwanufaishe na kuwainui kiuchumi.
Akizungumza na wananchi waliofaidika na mpango huo wa
Tasaf kata ya Sombetini na Daraja mbili amesema kuwa ni vema fedha hizo
zikawasaidie kwa kuanzisha biashara ndogo ndogo kufanya ufugaji na kuweka akiba
ya baadae.
“Serikali inataka wananchi wote waishi maisha mazuri
lakini haina huo uwezo kwa mara moja cha msingi kwa sisi ambao tumebahatika nah
ii Program ya TASAF awamu ya tatu hizi pesa tukazitumie vizuri ukichukua elfu
20 ukaenda kununua kanga sasa wewe utakuwa unatusaliti lakini nenda kanunue
nyanya,kama ni mboga za majani fanya biashara zitakusaidia kwenye maisha yako”Alisema
Dc Daqaro
Hata hivyo Daqaro amewasisita wataalamu wa maendeleo ya
jamii na wenyeviti wa mitaa pamoja na watendaji kuwasaidia wananchi kwa kupita
kwa kuwa karibu nao na kuwasilkiliza ili shida zao zitatuliwe mapema zaidi na
kwa wakati.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi walionufaika na mpango
huo wa Tasaf Bi Monica Thomas amemshukuru mkuu wa wilaya kwa kuwatembelea na
kuwakabidhi fedha hizo na amemuomba afikishe salamu kwa Raisi Magufuli kwa
kuwajali maskini.
Amesema kuwa fedha hizo zimewasaidia kwa kuwa wamepata
mitaji na kuanzisha biashara kama mama ntilie na kufuga kuku hivyo kwasasa wana
uwezo wa kupata milo mitatu na kuwapeleka watoto shule.
Naye mratibu wa TASAF jiji la Arusha Bi Tajiel Mahega
amesema kuwa mpango huo ni kwa ajili ya mitaa 70 ambapo wamefikia kaya 4773 na zaidi
ya shilingi milioni 100 zimetolewa.
DC DAQARO "FEDHA ZA TASAF MNAZOPEWA ZIKAWAONDOE KATIKA UMASKINI"
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment