Watu wapatao 247 waliokuwa wakisafiria kwa
ndege ya jeshi wamefariki dunia baada ya ndege hiyo kuanguka karibu na kambi ya
jeshi ya Boufarik nje kidogo ya jiji la Algiers, vyombo vya habari vimeripoti
Ripoti za vyombo vya habari zinasema ndege
hiyo aina ya Ilyushin Il-76, ilikuwa imewabeba askari kadhaa
Mtandao wa Algerie24, umeripoti kwamba ndege
hiyo ilikuwa inaelekea katika mji wa Magharibi wa Bechar
Picha zilizowekwa kwenye mtandao huo
zimeonyesha moshi mzito ukifuka kutoka eneo ambalo ndege hiyo imeangukia huku
watu wakikimbilia kutoa msaada
Tukio la ndege hiyo kuanguka Boufarik ndiyo
baya zaidi kwa Algeria tangu mwaka 2003 wakati ndege ya Shirika la Air Algerie
ilipoanguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa Tamanrasset na iliua
watu 102
Mwaka 2014, zaidi ya wanajeshi 70 pamoja na
familia zao walikufa pale ndege ya C-130 ilipoanguka kwenye milima ya Djebel Fertas
muda mfupi kabla ya kutua kwenye mji wa Kaskazini wa Constantine
Desemba 2012, ndege mbili za kijeshi
zilizokuwa zinafanya mazoezi ya kawaida ziligongana angani karibu na mji wa
Tlemcen ulioko Kaskazini Magharibi na kuua marubani wa ndege zote mbili.
Watu 247 wafa kwa ajali ya ndege Algeria
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment