Wasichana 5,900 wa umri chini ya miaka 18 wapachikwa mimba Tabora

Tabora. Watoto wa kike 5,913, wenye umri chini ya miaka 18 mkoani Tabora, wamebainika kupata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi Machi mwaka huu

Kauli hiyo imetolewa leo mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akifungua semina ya siku moja ya Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi ya Mkoa huo

Akizungumza leo Aprili 20 katika semina hiyo, Mwanri amesema:  “Takwimu hizo zinasikitisha na zinaonyesha kuwa bado kuna tatizo kubwa la watu wazima kukatisha ndoto za watoto wa kike mkoani humo.”

Mwanri amesema Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, inaongoza kwa wasichana 1,438 wenye umri wa chini ya miaka 18, kupata mimba

Nyingine ni Igunga (995) Kaliua (894), Sikonge (743) Uyui (640), Urambo (630), Manispaa ya Tabora (530) na Nzega Mjini (49)

Amesema vitendo hivyo si tu vinarudisha nyuma maendeleo ya watoto bali vinawaweka katika hatari ya kupata saratani ya mlango wa kizazi kwa kuwa wanashiriki ngono katika umri mdogo

Mwanri amewaagiza viongozi na watendaji katika Mkoa wa Tabora kuwafuatilia na kuwachukulia hatua haraka watu wote waliohusika na ujauzito wa watoto hao ili waweze kufikishwa katika vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazowakabili.
Wasichana 5,900 wa umri chini ya miaka 18 wapachikwa mimba Tabora Wasichana 5,900 wa umri chini ya miaka 18 wapachikwa mimba Tabora Reviewed by KUSAGANEWS on April 21, 2018 Rating: 5

No comments: