Dar es Salaam.
Msanii wa filamu Juma Chikoka maarufu kama 'Chopa wa Mchopanga' anayedai
ameshuhudia dakika za mwisho za kupigania uhai wake msanii wa muziki ‘Video
Queen’, Agnes Gerald, maarufu Masogange' amesema mrembo huyo amemuachia ujumbe
mzito ambao atausema siku ya mazishi
Chopa
ameyasema hayo jana wakati wa kikao cha dharura cha wasanii kuhusu maandalizi
ya mazishi yake yanayotarajiwa kufanyika Jumatatu Jijini Mbeya ingawa ataagwa
kwenye viwanja vya Leaders Jijini Dar es Salaam kesho
Msanii huyo
ambaye ni mmoja wa marafiki wa karibu wa Masogange, amesema dakika chache
kabla hajafariki alikuwa kalala mapajani kwake na walizungumza vitu vingi
ikiwemo kumpa ujumbe wa kuwaeleza Watanzania.
“Tuliongea
mengi lakini kuna makubwa mawili ambayo aliniagiza niwaambie Watanzania, ila
hilo nitalifanya kwa kuongea na vyombo vya habari na kuona namna sahihi ya
kusaidiana kama vijana, hatupaswi kuingizana katika matatizo
“Kwa sasa siwezi
kusema alichoniambia, embu ngoja tumalize shughuli ya kumhifadhi halafu
nitayaweka wazi aliyoniambia, kwani kwa sasa haitaleta picha nzuri na watu
wanaweza kutafsiri ndivyo sivyo,”amesema
Chopa amesoma
alikuwa akimtembelea Masogange, tangu alazwe katika Hospitali ya Mama Ngoma.
Amesema alilazwa hospitali kwa siku nne
“Ugonjwa
uliokuwa unamsumbua mbali na pumu, pia kupungukiwa damu, jana (juzi) nilikuwa
nimejipanga kwa ajili ya kumtolea damu lakini ndio hivyo hakuweza kumaliza
siku,” amesema
Msanii huyo
anasema amefahamiana na Masogange wakati akiwa Agnes Gerald na si Masogange,
urafiki ambao umedumu hadi mauti yanamfika.
Mchopanga: Nina siri nzito ya Masogange
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 21, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment