Siku moja baada ya msanii
anayepamba video za muziki wa Bongo Fleva nchini, Agness Gerald, maarufu
Masogange, kufariki dunia dada yake amesema wataifuata ratiba ya msiba kama
ilvyopangwa na wasanii wenzake
Akizungumza leo Aprili 21 dada wa
marehemu, Flora Gerald amesema, wataifuata ratiba ya msiba huo kwa hapa Dar
es Salaam, kama wasanii wenzake walivyosema
“Kama wenzake walivyosema, ataagwa
viwanja vya Leaders kesho na baada ya hapo atasafirishwa kwenda Mbeya na
Jumatatu atazikwa nyumbani kwa baba yake,” amesema
Hata hivyo Flora hakuweza
kuzungumza kwa kina kutokana na kujawa na majonzi
Mpaka saa nane mchana leo, wasanii
waliojitokeza wenye majina makubwa walikuwa ni Dogo Janja na Irine Uwoya
ambaye anaishi nyumba aliyokuwa anaishi Masogange
Jana Steve Nyerere alizungumza amesema kuwa Masogange ataagwa kesho na kusafirishwa kwenda
Mbeya kwa maziko.
|
|
Dada wa Masogange asema atakapozikwa Masogange
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 21, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment