Wananchi wachangia lita 164 za damu

Jumla ya lita 164 za damu zimepatikana   katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera baada ya wananchi wengi kujitokeza kuchangia damu kwa hiari

Lengo la kuchangia damu hiyo imedaiwa kwamba ni  kusaidia wagonjwa walioko katika hospitali za Nyamiaga, Murugwanza na Rulenge wanaohitaji huduma hiyo

Mratibu wa maabara  na damu salama  wilayani Ngara Mugisha Lubagola ametoa taarifa hizo leo Aprili 8 baada ya zoezi hilo kufanyika katika uwanja wa michezo wa kokoto ambapo uhamasishaji wa kuchangia damu umefanywa na Radio Kwizera mjini Ngara kupitia Kipindi cha Asubuhi njema

Lubagola amesema  damu hiyo itasaidia wagonjwa wanaopata ajali, watoto wachanga, na akina mama wanaojifungua wakiwemo wa upasuaji katika hospitali hizo japo haiwezi kukidhi mahitaji kwa mwezi katika Hospitali  na vituo vya Afya

Amesema  wilaya hiyo inahitaji lita  290 kila mwezi lakini zinazopatikana kwa watu kuchangia damu ni kati ya  lita 70 mpaka 85

Amesema wanalazimika kwenda kuazima damu kutoka wilaya jirani za Karagwe , Biharamulo na Misenyi

“Watu wanahitaji damu kutokana na mwili kushindwa kutengeneza chembechembe nyekundu za damu, ambayo kazi yake ni kusafirisha Oksijeni na kuweza kufanya kazi kuendelea kupumua na kuishi”Amesema Lubagol
Amesema  binadamu ili amchangie mwenzake damu lazima awe na umri wa miaka 18 mpaka 65 na achangie kila baada ya miezi mitatu, awe na afya bila kuwa na magonjwa kama kisukari ambapo siku ya kutoa damu asiwe na ugonjwa wa shinikizo la damu (presha
Aidha Kaimu  mratibu wa uhamazishaji  na mwendeshaji wa kipindi cha Asubuhi njema Radio Kwizera Boazi Zobanya, amesema   mwaka jana ulifanyika utafiti  mikoa sita ya kanda ya ziwa yenye  watu milioni 10, wanatakiwa kutumia unit 110,000
Zobanya amesema kwa mwaka jana baada ya kufanya utafiti  katika mikoa ya  Kagera, Kigoma Geita, Mwanza, Mara Shinyanga Simiyu na Tabora  ilibainika ukusanyaji wa damu ulikuwa lita  lita 51,000  sawa na asilimia 40 ya mahitaji
“Ilitajwa ufinyu wa bajeti na watu   kutoelimishwa kuhusu umuhimu wa kuchangia damu ni miongoni mwa changamoto zinazosababisha kuwepo kwa vifo vingi vinavyotokea kutokana  na uhaba wa damu”amesema Zobanya.  

“Damu tunayoipata inapelekwa kwenye maabara ya vipimo vya  Hospitali ya Bugando na kubaini Makundi ya  kumpatia mgonjwa kwa maana kila mtu analo kundi la damu linalomstahili kwenye mwili”Amesema


Wananchi wachangia lita 164 za damu Wananchi wachangia lita 164 za damu Reviewed by KUSAGANEWS on April 08, 2018 Rating: 5

No comments: