Watu watatu kati ya sita waliotoweka katika mazingira ya
kutatanisha usiku wa kuamkia Ijumaa Aprili 6, 2018 katika Kijiji cha Mitambuuni
shehia ya Mtambwe, Mkoa wa Kaskazini Pemba wameonekana alfajiri ya leo Jumapili
Aprili 8, 2018
Wameonekana katika Kijiji cha Mkungu Jimbo la Mtambile wilayani
Mkoani
Akizungumza kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Sheikhan
Mohamed Sheikhan amethibitisha kupatikana kwa watu
Amewataja vijana waliopatikana kuwa ni Said Shanani Mohamed (16),
Juma Kombo Fimbo (17) na Abdallah Khamis Abdallah (19
Imeelezwa vijana hao walionekana alfajiri, wawili kati yao
mikononi wakiwa na kamba
Amesema taarifa zaidi itatolewa baadaye na kamanda wa Mkoa wa
Kaskazini ambako ndiko walikotoweka
“Kwa sasa jeshi linafanya kazi na taarifa rasmi itatolewa kwenu na
jamii kwa jumla hapo baadaye,’’ amesema kamanda Sheikhan
Amewataka wananchi kushirikiana na Polisi kwa kutoa taarifa
zinazoashiria uhalifu
Vijana watatu waliotoweka Pemba wapatikana
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 08, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment