Mwandishi wetu,Arusha
Sekta ya Utalii nchini, inakabiliwa na uhaba wa wafanyakazi wenye
sifa hatua inayochangia, kushindwa kupambana na mataifa mengine katika
kuvutia watalii hivyo serikali na vyuo vinavyotoa elimu ya Utalii,
wameombwa kuboresha mitaala ili kwendana na mahitaji katika soko la
ajira.
Katibu Mtendaji wa chama cha waajiri katika nchi za Afrika ya
Mashariki(EAEO) Dk Aggrey Mlimuka, akizungumzia tatizo la uhaba wa wafanyakazi
wa sifa linazikabili nchi zote za afrika ya Mashariki alisema, nusu wa
wahitimu wa vyuo vikuu katika nchi hizo, hawana sifa stahiki katika soko la
ajira.
Katika kukabiliana na tatizo hilo,Mwekezaji wa Hoteli za Chem
chem, katika eneo la hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Burunge, wilayani
Babati, ameamua kuanza kuwafunisha wafanyakazi wake 160.
Meneja wa Chemchem Foundation, Charles Sylivesta alisema, wameamua
kuwafundisha wafanyakazi,kulingana na mahitaji ya idara zao ili kuwaongezea
uwezo wa kufanyakazi hasa kuhudumia watalii.
"wanafundishwa kiingereza,ubishi, kuandaa Vyumba vya kulala
watali na kuongoza watalii na tuna wataalam wa ndani na nje ya
nchi"alisema.
Meneja wa Chemchem Lodge Kelly Ricklan alisema mafunzo hayo,
yatasaidia wafanyakazi wao ambao wengi wao wanaishi katika eneo la
Burunge kupata uwezo wa kufanyakazi vizuri.
Akizungumza katika mafunzo hayo, Mwalimu wa lugha katika
hoteli hizo,John Macha alisema, baadhi ya wafanyakazi wamekuwa wakikabiliwa na
wakati mgumu kuwasiliana na watalii.
"kipindi hiki hatuna wageni wengi, tumeamua kuwafundisha
lugha mbali mbali za kimataifa ili waweze kuwasiliana vyema lakini pia waapewa
mafunzo ya wataalam wengine"alisema
Mmoja wa wafanyakazi wa hoteli hizo,Happy Mtani alisema mafunzo
hayo, yamekuwa na msaada mkubwa kwao kwani inawasaidia kuoboresha utendaji wa
kazi zao.
Kuna Uhaba wa wafanyakazi wenye sifa sekta ya Utalii
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 08, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment