Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dk Frederick
Shoo, amewataka Wakristo kuwa wajasiri na wathubutu wa kukemea na kuonya
pindi yanapotokea maovu na matendo yasiyofaa katika jamii
Dk. Shoo ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa
hilo, amesema leo Aprili 8 kwamba anatamani kungekuwa na Wakristo wengi
wenye sauti na ujasiri wa kukemea na kuonya kwa kusema ndugu yangu
Mwogope Mungu
Shoo ameyasema hayo jana wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili
katika usharika wa Msaranga Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa hilo ambayo
imetanguliwa na Ufunguzi wa Nyumba ya Mtumishi, Uzinduzi wa mashine ya
kusaga na kukoboa pamoja na upandaji Miti
Dk.Shoo amesema katika dunia ya leo yenye watu wenye midomo
michafu, unafiki mkubwa, kiburi, wenye kukata tamaa, wanaokataa maonyo,
wasioona madhaifu yao na wasiotaka kutubu, kunahitajika wakristo ambao
watasimama na kutubutu kusema Ndugu yangu mwogope Mungu
Aidha Dk.Shoo amesema , Dunia inahitaji ushuhuda wa matendo mema,
hivyo wakristo wanapaswa kusimama imara na kuwa na ujasiri wa kuonya na
kuwaambia watu wamwogope Mungu
"Ndugu zangu Mungu anataka kuwatumia kutangaza ukuu
wake, na natamani leo, kungekuwa na Wakristo wengi wenye sauti,inayoweza
kusema ndugu yangu mwogope Mungu"amesema Dk Shoo
Aidha amesema anatamani pia kuwa na wakristo wenye ujasiri
na ambao wanakaa na kuishi kwa upendo, amani na maelewano na binadamu wenzao
bila ya kujali tofauti zao,ukabila,rangi au vyeo vyao
"Yesu anatafuta mtu wa kumtuma katika jamii akaubiri na
akaishi amani,upendo,maelewano na Haki, sasa wakristo tukubali kutumwa kwenda
kushuhudia mahali popote".
Amesema katika dunia ya leo kuna watu ambao wanajua kupanga
maneno ambayo wanaweza kusema wanahubiri habari za Yesu lakini maisha na
mienendo yao ni kinyume na hayana uhalisia na Mungu wanayemtaja
Shoo pia amewataka wananchi kutunza na kuyalinda
mazingira,hatua ambayo itasaidia kuwepo kwa maji ya kutosha katika vyanzo na
kuepusha kuwepo kwa tatizo la upungufu wa maji
Ibada hiyo mbali na Askofu, pia ilihudhuriwa na viongozi
mbalimbali akiwemo msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa hilo,
Mwekahazina wa Dayosisi Exaudi Makyao, Mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro Kati,
Kenedi Kisanga, pamoja na wachungaji mbalimbali na viongozi wa Serikali.
Dk Shoo awataka wakristo kujijengea ujasiri
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 08, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment