Rais John Magufuli amewataka
viongozi wa madhehebu ya dini kuhubiri na kusisitiza amani ambayo ni msingi
wa maendeleo
Amesema hayo leo Aprili 8 katika
misa ya kusimikwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Isaac Amani
iliyofanyika katika parokia ya mtakatifu Theresia mjini humo
Amenukuu maandiko matakatifu
kutoka kwenye vitabu mbalimbali vya biblia yanayosisitiza amani
Kuhusu maombi matatu yaliyotolewa
na Padri Aloyce juu ya kuhamishwa Shule ya Msingi Naura ambayo ilianzishwa
mwaka 1950 ikiitwa St Theresa School mali ya Kanisa hilo ambayo ilitaifishwa
na Serikali mwaka 1967 alisema suala hilo lina changamoto kulipatia majibu ya
haraka
"Nikitoa tamko la kurejesha
shule hii leo litasumbua sana kila mali zilizotaifishwa mwaka 1967 zitatakiwa
kurejeshwa nami sitaki mgogoro huu," alisema Rais Magufuli
"Alisema anaamini kila jambo
lina wakati wake na waendelee kumuombea ili apate amani ya kutoa uamuzi
sahihi
Amesema hata suala la Shule ya
Saint Jude inayotoa elimu bure kwa watoto wanaotoka kwenye Kaya zisizo na
uwezo inayodaiwa kodi ya Sh6bilioni alisema hawezi kuingilia suala hilo
kwakua lipo mahakamani na hataki kuonekana anavunja sheria
Akizungumzia shughuli za maendeleo
katika jiji la Arusha alisema kumekua na mafanikio makubwa katika huduma za
elimu na afya
Kwa upande wake Askofu Mkuu
na Balozi wa Papa nchini, Maleck Schosist alitoa salamu zake na kumtaka
Askofu Mkuu ,Amani kufanya kazi ya utume.
|
Amani ukiiacha mbali hufanikiwi - Magufuli
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 08, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment