Wafuasi 24 wa chadema waliokamatwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar
es Salaam Jumanne iliyopita wameripoti Kituo Kikuu cha Polisi leo
Jumatano Aprili 11, 2018
Akizungumza nje ya kituo hicho, Ofisa wa
Kanda ya Pwani Chadema, Jerry Karege amesema waliitikia wito wa polisi na
walipofika
walielezwa kuripoti kwa mkuu wa upelelezi wa polisi mkoa wa
Ilala
Karege amesema walipofika kwa mkuu huyo wa
upelelezi walitakiwa kuripoti tena kituoni hapo Aprili 13 mwaka huu
"Sisi tumeitikia wito wa polisi lakini
hatujaambiwa kitu chochote zaidi ya kutakiwa kuondoka na kuripoti tena siku ya
Ijumaa,” amesema Karege.
WAFUASI 24 WA CHADEMA WARIPOTI POLISI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment