Majaji wawili wa
Mahakama ya Katiba nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamejiuzulu kwenye
nafasi zao, na kusalia majaji sita badala ya tisa katika Mahakama hiyo.
Jaji mmoja alifariki dunia siku ya
Jumapili na wengine wawili wamejiuzulu bila hata kutoa maelezo au sababu
ya kujuzulu kwao.
Majaji hao ambao ni Jean-Louis
Esambo na Banyaku Luape wamedaiwa kutoripoti katika Mahakama ya Katiba, Mnamo
Oktoba 17, 2016, ambayo ingetoa uamuzi muhimu kuhusu hatma ya DRC.
Imeelezwa kwamba Tangazo hilo limeishangaza
serikali ya DRC kwa uamuzi huo ingawa majaji hao wawili walionesha zaidi
ya mara moja maoni tofauti na rais wa mahakama hiyo.
Majaji wawili wajiuzulu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment