Viongozi watatu kati ya tisa wa Chadema tayari wamesharipoti
kituo kikuu cha polisi Dar es Salaam kama walivyotakiwa kuwa wanafanya
Viongozi hao pamoja na wabunge wanaokabiliwa na mashtaka
katika kesi namba 112/2018 iliyoko Mahakama ya Kisutu, wameripoti Ofisi ya
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya masharti ya
dhamana ya kesi hiyo
Ambao tayari wameshawasili ni Katibu Mkuu, Dk Vicent
Mashinji, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake(Bawacha), Halima Mdee na Mbunge wa
Bunda Mjini, Ester Bulaya
Viongozi hao wamekuwa wakitakiwa kuripoti polisi kama sehemu
ya dhamana yao katika kesi inayowakabili polisi"
Viongozi watatu wa Chadema wafika polisi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment