Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo
ya Makazi, William Lukuvi amezitaka halmashauri kutenga fedha za kutosha kila mwaka
kwa ajili ya mipango ya matumizi ya ardhi
Lukuvi amesema
mipango itasaidia kupanga na kupima kila kipande cha ardhi nchini kwa wakati
Amesema wizara
imeweka mikakati kuhakikisha ardhi yote ya Tanzania inapangwa, kupimwa na
kumilikishwa kisheria
Mikakati
inahusisha kuandaa programu ya kupanga, kupima na kumilikishwa kila kipande cha
ardhi nchini,” amesema Lukuvi leo Aprili 20, 2018
Waziri Lukuvi
alikuwa akijibu swali la mbunge wa Karatu, Willy Qambalo aliyetaka kujua
mkakati wa Serikali katika kuhakikisha ardhi yote ya Tanzania inapangwa na
kupimwa kisheria ili kuondoa migogoro
Lukuvi amesema
Serikali inatambua umuhimu wa kupanga mipango ya matumizi bora ya ardhi nchini
kama namna mojawapo ya kupunguza migogoro ya watumiaji na hasa wakulima na
wafugaji
Lukuvi atoa kauli fedha za mipango ya matumizi ya ardhi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment