Majaji wapya
walioapishwa mbali ya kuhimizwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma,
wametakiwa kuzisoma na kuzitafsiri vyema sheria kwani kama watafanya vinginevyo
wanaweza kuipoteza nchi
Kamishna wa
Maadili, Sekretarieti ya Maadili kwa Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold
Nsekela amewaambia majaji hao leo Ijumaa Aprili 20 Ikulu kuwa kazi waliyopewa
inahitaji umakini na uadilifu
“Someni sheria
na kuzitafsiri vizuri... Mahakama ndiyo chombo pekee kinachotafsiri sheria na
kama mtatafsiri vibaya mnaweza kuipoteza nchi,” amesema jaji huyo wakati akitoa
nasaha zake baada ya majaji hao wapya kuapishwa na Rais John Magufuli
Alisisitiza
kuwa katika utendaji wa kazi kumekuwa na mgawanyiko wa majukumu wakati Bunge
likitunga sheria, Serikali kazi yake kubwa ni kupendekeza sheria hizo
“Mahakama
ndiyo inayotoa tafsiri hivyo ili kuifanya vyema kazi hiyo lazima mtapaswa
kusoma sana na someni kwa makini maana kile mnachokiamua nyinyi ndiyo mwongozo
wa mwisho mpaka pale Bunge litakapoamua kutunga sheria nyingine,” amesema
Kuhusu kuishi
kwa uadilifu kamishna huyo aliwataka majaji hao kujichunguza mienendo mibovu
itakayoweza kuwaondoelea heshima kwa jamii
“Chagueni
vyema marafiki zenu ikiwezekana achaneni na wale wanaoonekana kutokuwa wema...
na ikiwezekana ukitoka zao kazini nenda nyumbani na siku kama ya leo Ijumaa
nenda msikitini kwa wale Waislamu na wale Wakristo nendeni kanisani Jumapili
... mnaweza kwenda pia kwenye burudani lakini angalieni burudani mnazokwenda,”
amesema
Rais Magufuli
leo amewaapisha majaji wapya kumi, wakili mkuu wa serikali na naibu wake na
naibu mkurugenzi wa mashtaka
Sherehe za
kuwaapisha majaji hao zinafanyika Ikulu na zinahudhuriwa na wageni mbalimbali
akiwamo Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi na Jaji Mkuu,
Profesa Ibrahim Juma.
Majaji wapya watakiwa kufuata sheria
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment