Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa katika ripoti ambayo alipokea kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad haikuwa na upotevu wa hizo fedha na kusema kama ungekuwepo angechukua hatua kali kwa wahusika siku hiyo hiyo.
Rais Magufuli amesema hayo leo April
20, 2018 wakati akiwaapisha majaji Ikulu Dar es Salaam na kusema kuwa watu
wanatumia uhuru wao vibaya na kupotosha watu kuhusu upotevu wa fedha hizo na
kuleta taharuki katika nchi.
"Kuna mtu anasema kwamba
imeibwa trilioni 1.5 siku moja nikampigia simu Controller and Auditor General
(CAG) kwamba mbona kwenye ripoti yako uliyonisomea hapa Ikulu hukunieleza juu
wizi wa Trilioni 1.5 kwa sababu ungenisomea hapo siku hiyo hiyo ningefukuza
watu , kama nimefukuza wakurugenzi watatu siku hiyo kwa kupata hati chafu hawa
na Trilioni 1.5 uliwaficha wapi nimejaribu kusoma ripoti yako nimeperuzi kila
kona sioni mahali zimeandikwa zimepotea trilioni 1.5 na Profesa Assad
akaniambia hakuna kitu kama hicho na Katibu Mkuu akasema hakuna trilioni 1.5
iliyoibiwa na serikali"
alisema Rais Magufuli
Aidha Rais Magufuli aliendelea
kusisitiza kuwa
"Kwa sababu ya uhuru wa mtu
kuandika chochote kwenye mitandao kwani hata ndege walisema mbovu hivyo ni
kawaida ya uhuru huu, bahati nzuri Controller and Auditor General yupo hapa eti
Controller and Auditor General kwenye ripoti yako tumeibiwa Trilioni 1.5? Sema
hapa hapa watu wajue"
Alisimama CAG akiwa Ikulu jijini Dar
es Salaam na kusema hakuna kitu kama hicho hata Katibu Mkuu pia alisimama na
kusema hakuna jambo kama hilo na kusisitiza kuwa Hazina wapo vizuri na wapo
salama kabisa.
Rais Magufuli awanyanyua CAG, Katibu Mkuu kujibu suala la Sh1.5 trilioni
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment