Rais Magufuli awanyanyua CAG, Katibu Mkuu kujibu suala la Sh1.5 trilioni


Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa katika ripoti ambayo alipokea kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad haikuwa na upotevu wa hizo fedha na kusema kama ungekuwepo angechukua hatua kali kwa wahusika siku hiyo hiyo.  

Rais Magufuli amesema hayo leo April 20, 2018 wakati akiwaapisha majaji Ikulu Dar es Salaam na kusema kuwa watu wanatumia uhuru wao vibaya na kupotosha watu kuhusu upotevu wa fedha hizo na kuleta taharuki katika nchi. 

"Kuna mtu anasema kwamba imeibwa trilioni 1.5 siku moja nikampigia simu Controller and Auditor General (CAG) kwamba mbona kwenye ripoti yako uliyonisomea hapa Ikulu hukunieleza juu wizi wa Trilioni 1.5 kwa sababu ungenisomea hapo siku hiyo hiyo ningefukuza watu , kama nimefukuza wakurugenzi watatu siku hiyo kwa kupata hati chafu hawa na Trilioni 1.5 uliwaficha wapi nimejaribu kusoma ripoti yako nimeperuzi kila kona sioni mahali zimeandikwa zimepotea trilioni 1.5 na Profesa Assad akaniambia hakuna kitu kama hicho na Katibu Mkuu akasema hakuna trilioni 1.5 iliyoibiwa na serikali" alisema Rais Magufuli 

Aidha Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kuwa

"Kwa sababu ya uhuru wa mtu kuandika chochote kwenye mitandao kwani hata ndege walisema mbovu hivyo ni kawaida ya uhuru huu, bahati nzuri Controller and Auditor General yupo hapa eti Controller and Auditor General kwenye ripoti yako tumeibiwa Trilioni 1.5? Sema hapa hapa watu wajue" 

Alisimama CAG akiwa Ikulu jijini Dar es Salaam na kusema hakuna kitu kama hicho hata Katibu Mkuu pia alisimama na kusema hakuna jambo kama hilo na kusisitiza kuwa Hazina wapo vizuri na wapo salama kabisa. 


Rais Magufuli awanyanyua CAG, Katibu Mkuu kujibu suala la Sh1.5 trilioni Rais Magufuli awanyanyua CAG, Katibu Mkuu kujibu suala la Sh1.5 trilioni Reviewed by KUSAGANEWS on April 20, 2018 Rating: 5

No comments: