Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu amewashukuru
Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupitisha bajeti ya wizara
yake kwa mwaka 2018/19.
''Nawashukuru Wabunge kwa kupitisha
Bajeti ya Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii kwa mwaka 2018/19'', amesema Mh.
Ummy siku moja baada ya bunge la bajeti kwa pamoja kupitisha bajeti hiyo.
Mbali na shukrani hizo Mh. Ummy pia
ameahidi kufanyia kazi ushauri ambao umetolewa na wabunge hususani kwenye
uboreshaji wa huduma za afya pamoja na miundombinu yake nchini kote.
''Tutafanyia kazi maoni na ushauri
wenu ili kuboresha huduma za Afya na Ustawi wa jamii nchini hasa kwa wananchi
wa kipato cha chini katika maeneo ya vijijini ili waweze kunufaika na bajeti
hii'', ameongeza.
Vipaumbele vya bajeti ya wizara hiyo
ambayo imetengewa jumla ya shilingi bilioni 898 ni Chanjo, Kinga, Magonjwa
yasiyoambukiza, Afya ya uzazi, Damu salama, Dawa na vifaa tiba, Hospitali za
Mikoa na Kanda pamoja na Vituo vya Afya.
Ummy awashukuru wabunge kwa bilioni 898
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 21, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment