Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amefunguka na kudai kuna baadhi ya
wananchi hususani wanaoishi mijini hawana desturi ya kuhifadhi chakula cha
akiba majumbani mwao jambo ambalo ni baya linaweza kuhatarisha maisha yao kwani
hata panya na mchwa huwa wanahifadhi
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo
Aprili 21, 2018 wakati alipokuwa anatoa salamu za kwa wananchi wa mkoa wa
Dodoma waliojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa mradi
maghala na vihenge vya kisasa kwa ajili ya kuhifadhia chakula lenye uwezo wa
kubeba tani elfu 20.
"Binadamu asiyekuwa na akiba ya
chakula atakuwa waajabu sana, kama mchwa na panya wanaweka akiba ya vyakula je
itakuja kuwa binadamu ?. Sisi watu wa mijini tukikaguliwa nyumba zetu hata debe
ndani la mahindi hukuti wala nusu debe ya maharage kazi ni kwenda sokoni kila
siku", amesema Ndugai.
Kwa upande mwingine, Spika wa Bunge
Job Ndugai amempongeza Rais wa awamu ya tano Dkt. John Magufuli pamoja na
wasaidizi wake akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kuweza kutekeleza ahadi
zilizopo kwenye Chama cha Mapinduzi (CCM).
"Binadamu asiyekuwa na akiba ni waajabu"- Spika
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 21, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment