Spika Ndugai: Tundu Lissu alikwenda kutibiwa Nairobi bila kufuata utaratibu wa Bunge



SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema Bunge haliwezi kuidhinisha fedha kwa ajili ya matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa kuwa halijapata vibali vitatu.
Ndugai ametoa msimamo huo leo bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge Godbless Lema kuomba mwongozo wa kutaka kujua sababu za Bunge kutogharamia matibabu ya mbunge huyo wa upinzani.  
Kwa mujibu wa Spika Ndugai, vibali vinavyohitajika ni pamoja na barua kutoka kwa Rais, kibali kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto na Hospitali ya Taifa, Muhimbili.  
“Bila Bunge kupata vibali vitatu, Bunge haliwezi kuandika check (hundi),” amesema Spika Ndugai.
Amesema, wabunge wana namna mbili ya kupata matibabu ikiwemo kutumia kadi ya matibabu ya NHIF ndani ya nchi pekee na kutibiwa nje ya nchi kwa vibali muhimu.
Ameushukuru Ubalozi wa Ujerumani ambao umemhakikishia kuwa ndiyo unaofadhili matibabu ya Tundu Lissu huko Ujerumani.  

“Tunawashukuru wenzetu wa Ujerumani kwa msaada wanaoutoa kumtibu Lissu huko Ubeligiji. Nilikutana na Balozi wa Ujerumani na kunieleza hili,” amesema.

Spika Ndugai: Tundu Lissu alikwenda kutibiwa Nairobi bila kufuata utaratibu wa Bunge Spika Ndugai: Tundu Lissu alikwenda kutibiwa Nairobi bila kufuata utaratibu wa Bunge Reviewed by KUSAGANEWS on April 19, 2018 Rating: 5

No comments: