Spika wa Bunge, Job Ndugai ametaka kina mama
wenye malalamiko ya kutelekezewa watoto na wabunge wafike kwake au wamwandikie
barua kuhusu suala hilo
Hata hivyo, amesema watakapofanya hivyo
wapeleke na cheti cha uthibitisho cha vipimo vya vinasaba (DNA) ili waone ni
namna gani ya kushughulikia suala hilo
Ndugai alisema hayo jana Jumanne Aprili 10,
2018 kabla ya kuahirisha kikao cha sita cha Bunge mjini Dodoma.
Katika kauli yake iliyoambatana na vicheko
Spika alisema, “Kule Dar es Salaam kuna zoezi linaendelea, huko sasa kidogo
kiti cha Spika kimetikiswa hivi. Tunatuhumiwa mahali, kidogo tumeguswa hivi kwa
hiyo natarajia kupata ushauri wenu waheshimiwa tunafanyaje katika mazingira
haya kwa maana kuna watoto wetu wako barabarani.”
“Haiwezekani hata kidogo, kwa hiyo kina mama
wale inabidi tufanye utaratibu tujue nini tutafanya lakini pia kuna kina baba
wamejitokeza huko nimesikia na baadhi ya walalamikiwa ni kina mama wabunge, kwa
hiyo hili jambo halina upande,” alisema Ndugai
“Hawa kina mama kama wapo, basi waje kwa
spika au wamwandikie spika lakini waniletee na DNA test certificate (cheti cha
uthibitisho cha vipimo vya vinasaba) ili tuone namna gani ya kuwezesha
“Kuna mafungu hapa tumepitisha tunaweza
kuangalia namna ya kuweka sawasawa ili waheshimiwa wabunge wawe na utulivu
katika kufanya kazi za Bunge na si kuwa na mawazo mengine,” alisema
Spika atoa neno kwa wanawake waliotelekezwa na wabunge
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment