Serikali imesema,
imefanikisha kuyashughulikia matukio 1,072 kwa mwaka 2017
yaliyoripitiwa kupita namba maalum iliyotolewa na Serikali kwa ajili ya
kuripoti matukio ya udhalilishaji na unyanyasi hususan Wanawake na Watoto.
Akizungumza leo Bungeni Mjini
Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto,
Dk. Faustine Ndugulile, amesema hiyo ni kati ya mikakati mingi iliyowekwa
na serikali kwa ajili ya kukomesha matukio ya udhalilishaji kwa watoto nchini.
Aidha, Dk. Ndungulile amesema,
Wizara yake tayari imeshatoa mafunzo kwa Maafisaa Maendeleo ya
Jamii na Ustawi wa Jamii wapatao 50 katika mikoa yote 26 kwa ajili ya kuanzisha
Kamati za Ulinzi kuanzia ngazi ya kijiji hadi Taifa ili kupunguza kama si kumaliza
kabisa tatizo hilo.
Serikali yafanikiwa baada ya kuweka mikakati hii
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment