Mbunge atoa siri ya kuua upinzani


Mbunge wa jimbo la Temeke (CUF), Abdallah Mtolea amedai kuwa kama mtu anataka kuviua vyama vingi vya siasa ni kutekeleza yale yote wananchi wanayoyahitaji ikiwa ni pamoja kutoa zile huduma stahiki.

Mh. Mtolea ameweka wazi hayo wakati akizungumza amesema iwapo wananchi watapatiwa yale ya msingi vyama vinavyoitwa vya upinzani vinaweza kukosa hoja ya kukosoa lakini siyo kuviua kabisa kwani hata huko Marekani ambapo wameshapigana kwa kiasi kikubwa na maadui watatu bado kuna vyama vingi kwa ajili ya kurekebishana.

Aidha Mbunge huyo ambaye yupo chini ya Mwamvuli wa UKAWA amesema kwamba licha ya Tanzania kwa sasa kutokuwa na uwanja mzuri wa kufanyia siasa lakini anaamini  kwa watu wanaoamini siasa za upinzani hata wakipewa nusu saa ya kufanya kazi hiyo itawatosha kabisa kwani ambacho wanachokizungumza kipo ndani ya jamii.

Ameongeza kwamba kuwa hatamani kusikia hata siku moja kwamba vyama vya upinzani  nchini vitakufa kwani watu kama yeye bado  wapo wanaoamini ndani ya upinzani .

"Sitamani kusikia kwamba vyama vya upinzani vinakufa.

Bado tupo sisi tunaoamini ndani ya upinzani na nina uhakika hata tukiachiwa nusu saa ya kuzungumza tutafanya tuu kwani yale tunayozungumza hayatoki hewani. Hata tukifunguliwa 2020 tukaambiwa fanyeni siasa itatosha maana siasa ni maisha ya kila siku ya mwananchi. Ukitaka kutuua tekeleza yale wanayoyataka kwani sisi tukiongea tunaonyesha yale makosa"- Mtolea

Mbunge atoa siri ya kuua upinzani Mbunge atoa siri ya kuua upinzani   Reviewed by KUSAGANEWS on April 05, 2018 Rating: 5

No comments: