Mbunge wa jimbo la
Temeke (CUF), Abdallah Mtolea amedai kuwa kama mtu anataka kuviua vyama vingi
vya siasa ni kutekeleza yale yote wananchi wanayoyahitaji ikiwa ni pamoja kutoa
zile huduma stahiki.
Mh. Mtolea ameweka wazi hayo wakati
akizungumza amesema iwapo wananchi watapatiwa yale ya msingi vyama
vinavyoitwa vya upinzani vinaweza kukosa hoja ya kukosoa lakini siyo kuviua
kabisa kwani hata huko Marekani ambapo wameshapigana kwa kiasi kikubwa na
maadui watatu bado kuna vyama vingi kwa ajili ya kurekebishana.
Aidha Mbunge huyo ambaye yupo chini
ya Mwamvuli wa UKAWA amesema kwamba licha ya Tanzania kwa sasa kutokuwa na
uwanja mzuri wa kufanyia siasa lakini anaamini kwa watu wanaoamini siasa
za upinzani hata wakipewa nusu saa ya kufanya kazi hiyo itawatosha kabisa kwani
ambacho wanachokizungumza kipo ndani ya jamii.
Ameongeza kwamba kuwa hatamani
kusikia hata siku moja kwamba vyama vya upinzani nchini vitakufa kwani
watu kama yeye bado wapo wanaoamini ndani ya upinzani .
"Sitamani kusikia kwamba vyama
vya upinzani vinakufa.
Bado tupo sisi tunaoamini ndani ya
upinzani na nina uhakika hata tukiachiwa nusu saa ya kuzungumza tutafanya tuu
kwani yale tunayozungumza hayatoki hewani. Hata tukifunguliwa 2020 tukaambiwa
fanyeni siasa itatosha maana siasa ni maisha ya kila siku ya mwananchi. Ukitaka
kutuua tekeleza yale wanayoyataka kwani sisi tukiongea tunaonyesha yale
makosa"- Mtolea
Mbunge atoa siri ya kuua upinzani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment