Kesi inayowakabili
viongozi wa juu wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na Geofrey Nyange 'Kaburu'
imeharishwa kwa mara nyingi tena leo hadi Aprili 12, 2018 kufuatilia ombi la
upande wa mashtaka kudai wanataka kumuongeza mshtakiwa mmoja katika kesi hiyo.
Hayo
yameelezwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam
Thomas Simba, na Wakili wa Serikali kutoka TAKUKURU, Leornad Swai na kusema
kesi hiyo ilifikishwa Mahakamani hapo kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo
ya awali baada ya upelelezi wa kesi yao kukamilika.
Hata hivyo,
Wakili Swai aliiomba Mahakama ahirisho fupi kwa kuwa wanatarajia kufanyia
mabadiliko katika hati ya mashtaka kwa kuongeza mshtakiwa mmoja.
Kufuatia ombi
hilo, Mahakama iliamua kuahirisha kesi hiyo hadi Aprili 12 mwaka 2018 kwa ajili
ya upande wa mashtaka kufanya mabadiliko yao na washtakiwa kusomewa maelezo ya
awali.
Aveva na
Kaburu kwa pamoja walipandishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza Juni 27 mwaka
2017 wakiwa wana kabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ikiwemo ya kughushi,
kuwasilisha nyaraka ya uongo na utakatishaji wa fedha.
Kesi ya Aveva na Kaburu aunganishwa mwingine
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment