RTO ARUSHA MADEREVA MSIJARIBU KUPIMA KINA CHA MAJI KWA KUTUMIA MAGARI YENU


Kamanda wa jeshi la Polisi usalama Barabarani Mkoani Arusha Charles Bukombe amewataka madereva wanaoendesha vyombo vya moto kuchukua tahadhari kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

Akizungumza na KUSAGANEWS Ofisi kwake Kamanda Bukombe amesema kuwa madereva wasijaribu kupimo cha maji kwa kutumia gari na kuepuka kuendesha kama wanaona kutatokea madhara.
“Madereva wawe makini wasijaribu kuyapima maji kwa kutumia gari unapona maji ni mengi ni vema uka paki Gari ni vema ukatest wewe kuliko ukaingiza gari “Amesema Bukombe

Pamoja na hayo amesema kuwa jeshi la polisi limejipanga kushughulikia madereva ambao wanaenda kinyume cha utaratibu ambapo kwasasa wanalipa faini kwa kutumia mashine kielekronic ambazo zinaonyesha taarifa za leseni za madereva ambao hawana sifa.

“Sasa hivi adhabu zinalipwa kwa kutumia mashine za electronic japo bado zile Manual zipo mashine zinapofeli tunatumia vitabu lakini zile mashine zinaonyesha data halisi za madereva inavyobainika madereva wengi wanaleseni za kufoji leseni yake class ni D ameenda sehemu akascan wakamuongezea Class C Ukiingiza kwenye System inasoma Class D au daraja la kuendesha pikipiki kabisa sasa niwatake tu madreva wenye leseni wanazozijua hizo wakikamatwa watashtakiwa kwa kosa la usalama barabarani lakini watahtakiwa kwa kosa la Fojari”Alisema Bukombe

RTO ARUSHA MADEREVA MSIJARIBU KUPIMA KINA CHA MAJI KWA KUTUMIA MAGARI YENU RTO ARUSHA MADEREVA MSIJARIBU KUPIMA KINA CHA MAJI KWA KUTUMIA MAGARI YENU Reviewed by KUSAGANEWS on April 19, 2018 Rating: 5

No comments: