JKCI yatibu wagonjwa 19,371 miezi mitatu


TAASISI ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa miezi mitatu ya Januari hadi Machi 2018 imehudumia wagonjwa 19,371 wenye matatizo ya moyo wakiwemo 890 waliolazwa.
Taarifa ya kitengo cha uhusiano cha taasisi hiyo, wagonjwa 105 wamefanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua wakiwemo watu wazima 53 na watoto 52.
Kati ya wagonjwa 105 waliofanyiwa upasuaji 66 wamefanyiwa na madaktari bingwa Watanzania. Madaktari hao wamefanya upasuaji wa watoto 35 na watu wazima 31.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, upasuaji wa moyo bila kufungua kifua kwa kutumia mtambo wa Cathlab ulifanyika kwa wagonjwa 231 wakiwemo watoto 20 na watu wazima 211. Imesema, kati ya wagonjwa 231 waliotibiwa watu wazima 211 walifanyiwa upasuaji na madaktari wa Tanzania.
“Kwa kipindi cha miezi mitatu tumekuwa na jumla ya kambi za matibabu nane (8) ambapo tulifanya matibabu kwa kushirikiana na washirika wetu kutoka nchi za Ujerumani, Israel, Australia, Marekani, India na Falme za Kiarabu” imesema taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, katika kambi hizo wagonjwa 39 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua wakiwemo watoto 17 na watu wazima 22. Wagonjwa 72 walifanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua wakiwemo watoto 20 na watu wazima 52.
“Tumefanya upasuaji wa kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis) 36”imesema.
Amesema, changamoto kubwa inayoikabili taasisi hiyo ni wagonjwa wengi mioyo yao kutokuwa kwenye hali nzuri hivyo amewaomba wananchi wawe na tabia ya kupima afya mara kwa mara ili wapate tiba kwa wakati.

JKCI yatibu wagonjwa 19,371 miezi mitatu JKCI yatibu wagonjwa 19,371 miezi mitatu Reviewed by KUSAGANEWS on April 19, 2018 Rating: 5

No comments: