Mkuu wa mkoa wa kilimanjaro Anna Mgwira amewataka Vijana
kuwa na tabia ya kuwajali na kuwatunza wazazi wao hasa pale wanapokuwa
wagonjwa.
Mgwira ametoa rai hiyo leo
wakati akitoa salamu za rambirambi kwenye msiba wa mama wa Mkuu wa Mkoa
wa Arusha Mrisho Gambo Bi Rehema Paulo uliofanyika wilaya ya Moshi
Vijijini kijiji cha Msumi mkoani Kilimanjaro ambapo amesema kuwa Vijana
wanapaswa kuiga mfano wa Gambo ambaye amemjali mama yeke hadi kufikia
mauti.
Akisoma wasifu wa marehemu
mwakilishi wa familia ya Gambo amesema kuwa marehemu Rehema Mumburi
amefariki dunia tarehe 12 nchini India akiwa na umri wa miaka 58 kutokana
na ugonjwa wa kisukari uliokuwa ukimsumbua toka awali na baadae kuanza
kusumbuliwa na figo na uvimbe uliosababisha damu kuvijia kwenye ubongo na
hatimaye madaktari wakiwa wanafanya jitihada za kuokoa maisha yake aliaga
dunia.
Aidha msiba huo umehudhuriwa mawaziri,
wakuu wa mikoa, wilaya, wabunge, Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini na
watu wengine wengi
RC MGWIRA ATOA NENO KWENYE MSIBA WA MAMA MZAZI WA RC GAMBO
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 19, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment